LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 24, 2015

KINANA AENDELEA NA ZIARA LEO YUPO JIMBO LA KWIMBA


  • Mwenyekiti wa Kijiji kutoka  Chadema ajiuzulu  nakujiunga na CCM
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kwimba Ndugu Petro Ngh'ingi wakati wa mapokezi kwenye kijiji cha Mwamaya kata ya Hungumalwa Pichani kati ni Katibu wa CCM Wilaya ya Kwimba Bi.Tabu Lugwesa.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Kwimba Mhe. Shanif Hilan Mansoor wakati wa mapokezi kwenye kijiji cha Mwamaya kata ya Hungumalwa wilaya ya kwimba mkoani Mwanza.
 Walinzi wa Jadi wa kisukuma maarufu kwa jina la Sungusungu wakimpokea Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye mavazi ya jadi ya walinzi wa Kisukuma maarufu kama Sungusungu.

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na wananchi wa kata ya hungumalwa waliojitokeza kwa wingi kumpokea Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye kijiji cha Mwamaya, Kwimba mkoani Mwanza.
 Mbunge wa Jimbo la Kwimba Mhe. Shanif Hilan Mansoor akihutubia wakazi wa kijiji cha Mwamaya wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mwamaya waliojitokeza kwa wingi kumpokea kwenye wilaya ya Kwimba, mkoani Mwanza.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasha umeme kama ishara ya kuwasha umeme  kwenye nyumba ya Ndugu Charles Lusana mkazi wa kijiji cha Mwamaya kata ya Hungumalwa,Kwimba mkoani Mwanza.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Ndugu Charles Lusanamkazi wa kijiji cha Mwamaya kata ya Hungumalwa mkoani Mwanza mara baada ya zoezi la kuwasha umeme kukamilika
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia kikundi cha ngoma za utamaduni Idibuili wakati alipotembelea kijiji cha Hungumalwa kuona na kushiriki ujenzi wa Zahanati.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokea kadi ya Chadema kutoka kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Ilula Hamala Materemki, kata ya ilula wilani Kwimba aliyejiuzulu na kuamua kujiunga na CCM.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Diwani ya kata ya Hungumalwa Shija Marando wakati wa kuona na kushiriki ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Hungumalwa.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wakazi wa kijiji cha Hungumalwa wakati wa kuona maendeleo ya ujenzi wa zahanati ya kijiji.Wengine pichani ni Mbunge wa jimbo la Kwimba Mhe. Shanif Hilan Mansoor na Diwani wa Kata ya Hungumalwa Shija Marando.
 Mbunge wa jimbo la Kwimba Mhe. Shanif Hilan Mansoor akishiriki ujenzi wa zahanati ya Hungumalwa wilayani Kwimba.
(Picha zote na Adam Mzee na Bashir Nkoromo)

KWA PICHA ZAIDI BOFYA

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages