LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

May 4, 2015

KATIBU MKUU WA UVCCM SIXTUS MAPUNDA AHARIBU MIPANGO YA WAPINZANI MKOANI IRINGA




 Katibu mkuu wa UVCCM taifa Sixtus Mapunda akiwapa maneno ya kishujaa wakazi wa mkoa wa Iringa
 Juliana Shonza akiwahutubia wananchi wa mkoa wa Iringa
 Viongozi Chama Cha Mapinduzi wakiwa katika meza wakifuatia mkutano unavyoendele

na fredy mgunda,iringa.

katibu mkuu wa uvccm taifa afanya ziara ya jimbo la kilolo kwa lengo la kukijenga chama  na kuangalia maendeleoya chama hicho  hasa ngazi vijana lakini akiwa katika ziara hiyo aliongozana na mwenyeji wake   katibu wa uvccm mkoa wa iringa.

akihutubia wakati wa mkutano uliofanyika katika kijiji cha kitumbuka kata ya ilole katibu wa uvccm mkoa wa iringa elisha mwampashi aliwataka wanachama wa chama hicho kuondoa unyonge dhidi ya wapinzani wake kwa kuwaambia ukweli wananchi juu ya maendeleo yanayofanywa na chama hicho.

aidha mwampashe amesema kuwa ifike wakati viongizi wa chama hicho kuacha kujidanganya kwa kuwapa taarifa viongozi  za matumaini juu ya maendeleo ya chama hicho.
“tunatakiwa tubadilika sasa kwa kuwapa taarifa za ukweli viongozi wetu ili wanapoondoka wajue  nini cha kufanya ili kuondoa dosari ambazo zinzkuwa zikijitokeza,tuenaelekea kwenye uchaguzi mkuu ambao utafanyika hapo “alisema mwampashe

kwa upande wake katibu wa uvccm taifa  sixtus mapunda amewapongeza wananchi na wanachama wa tarafa ya ilole kwa ujumla  kwa ushindi walioupata wakati wa serikali za mitaa ambao unaashilia chama hicho kuendelea kupendwa kata tarafa hiyo.

lakini mapunda aliwatoa hofu wananchi wa kijiji cha kitumbuka kwa kusema amesikia na kujionea baadhi ya matatizo yanayoikabili kata ya ilole na kuwaahidi kuyafikisha kwa mbunge wao na kutafuta njia ya kuyatatua kwa kuwa profesa petter msola ni msikivu.

“tatizo la kufikisha nguzo za umeme katika eneo hili ni tatizo dogo ambalo linatatulika kwa haraka na kuwaahidi wananchi kulifanyia kazi mapema ,suala la barabara alisema kuwa amejionea yeye mwenyewe kuwa  si nzuri na inahatarisha maisha kwa kuwa pindi mvua itakaponyesha barabara hiyo itakuwa kama mto”.alisema mapunda.




ALIYEKUWA  kada maarufu  wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema ) Taifa Juliana Shonza ambae alijiuzulu na chama hicho na kijiunga na CCM amewataka wakazi wa jimbo la Iringa mjini kuungana kulipokea jimbo kutoka kwa mbunge Mch Peter Msigwa.

Shonza ametoa kauli hiyo leo wakati akiwahutubia wakazi wa jimbo la Iringa mjini wakati wa mkutano wa uzinduzi wa matawi unaofanywa na katibu mkuu wa Uvccm Taifa sixtus Mapunda.

Alisema jimbo la Iringa mjini ni jimbo ambalo wananchi walichagua mbunge kwa hasira na kuwa badala ya kutegemea maendeleo wamejikuta wakifanya maandamano yasiyo na kikomo kila uchwao.

Shonza alisema kuwa mbunge wa jimbo la Iringa mjini amekuwa ni mtu wa kujipigania mwenyewe kimaisha badala ya kujishughulisha kuwaletea wananchi maendeleo.

Hivyo alisema ni vema wananchi wa Iringa mjini kujipanga kwa hafla ya kulipokea jimbo hilo kutoka kwa mpangaji mbunge Msigwa aliyepanga bila kujua kama kapangishwa hivyo kushindwa kulipa kodi.

Akielezea juu ya hofu ya muungano wa vyama vinavyounda katiba ya wananchi (ukawa) alisema kuwa Chadema ni chama ambachokinataka kupanda kupitia ukawa.

Kwani alisema Chadema ndio chama kilichokituhumu CUF kuwa ni CCM  B na kuwa ni chama cha kishoga imekuwa leo kuungana 

Hivyo kuwataka watanzania kupima na kutoa maamuzi magumu pindi uchaguzi utakapo fika.

Nae mjumbe wa kamati ya utekelezaji Uvccm Taifa Secky Kasuga alisema wananchi wa jimbo la Iringa walianzimisha jimbo hilo na sasa mwenye Nyumba anahitaji Nyumba Yake hivyo lazima mpangaji kuondoka.

"Tunalazimika kuchukua Nyumba yetu baada ya mpangaji kushindwa kufagia nyumba"

Katibu mkuu wa UVccm Taifa Sixtus Mapunda alisema kilio cha maendeleo kwa jimbo la Iringa kimetokana na mchanganyo uliofanywa na wananchi kwa kumchagua mbunge mrudisha nyuma maendeleo.

Alisema mbunge amekuwa kikwazo kikubwa kwani bungeni wakati wa vikao vya bajeti yeye anatoka nje ya bunge na wakati wa vikao vya kupanga shughuli za maendeleo halmashauri yeye anashiriki kuita maandamano.

" Tunawaombeni wana Iringa mtusaidie kurejesha jimbo kwa kumtoa mbunge mpinga maendeleo katika jimbo la Iringa mjini ambalo maendeleo yanaletwa kwa nguvu na ccm"

Bw Mapunda asema anawashangaa wapinzani kwa kuikataa katibu inayopendekezwa ambayo unazungumzia pia Haki ya kuishi hivyo  kupinga Kwao wanapinga hadi haki ya wao kuishi.

Alisema kuwa hoja Yao ni kutaka serikali tatu na si vinginevyo na kuwa wananchi lazima wapigie kura ya ndio katiba hiyo na pindi muda wa serikali tatu utakapofika basi itafanyika hivyo na si sasa.

Kuwa kuutaka utanganyika ni kuutaka ukoloni hivyo lazima kujitambua kuwa wakati wa kuongozwa na wakaloni umepita.






1 comment:

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages