LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 24, 2015

VIONGOZI WATAKIWA KUFANYA MAMBO WANAYOFANYA WANANCHI


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wajumbe wa halmashauri kuu ya wilaya ya Kusini,Katibu Mkuu yupo kwenye ziara ya kujenga na kuimarisha chama.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisukuma toroli kupeleka udongo kwenye ofisi yaJimbo Kitogani pamoja na Mbunge wa Jimbo la Muyuni Mhe. Dkt. Maadhi Juma Maalimu (Mb) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na viongozi wa CCM wilaya ya Kusini wakielekea katika Sheia ya Kibigija kukutana na wakulima wa Mwani.
 Mwakilishi wa Jimbo la Muyuni Jaku Hashim akizungumza na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kuhusu changamoto wanazokutana nazo wakulima wa mwani na namna wanavyosaidia.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupanda mwani pamoja na wakulima wa zao hilo Jambiani sheia ya Kibigija.Kinana aliwataka viongozi kushiriki yale wanayofanya wananchi kwani ndio njia pekee yakujua uzito wa changamoto zinazowakabili.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupanda mwani pamoja na wakulima wa zao hilo Jambiani sheia ya Kibigija.



Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimjulia hali Mwenyekiti mstaafu Haji Abdala Haji ambaye ni mgonjwa kwa sasa

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages