LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 10, 2014

MBUNGE WA JIMBO LA AMANI, ZANZIBAR, AWAELEZA VIONGOZI WA CHAMA JUU YA KATIBA.


VIONGOZI wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa Jimbo la Amani wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo hilo , Mhe. Mussa Hassan Mussa (hayupo pichani) wakati wa mkutano wa kuwapokea viongozi wa jimbo hilo baada ya kumaliza bunge maalum la Katiba lililomalizika mjini Dodoma mwezi uliopita, mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa Johari Yussuf Akida uliopo Amani mjini Zanzibar.(Picha na Haroub Hussein).

MBUNGE wa Jimbo la Amani, Mhe. Mussa Hassan Mussa akizungumza na viongozi wa Chama cha Mapinduzi wa jimbo hilo kuhusiana na suala la Katiba inayopendekezwa pamoja na kuwataka kutoa taaluma kwa wananchi juu ya katiba hiyo na kuwataka kuipigia kura ya ndio wakati wa kura ya maoni itakayofanyika mwakani, mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa Johari Yussuf Akida uliopo Amani mjini Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages