LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 29, 2014

KINANA AWEKA HISTORIA MTWARA MJINI

  • Apokelewa kwa Shangwe
  • Akagua miradi ya maendeleo
  • Ataka wana CCM kushikamana
  • Kuhutubia wakazi wa Mtwara kesho kwenye uwanja wa Mashujaa
 Vijana wa Bodaboda wakiongoza msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati akiwasili Mtwara mjini ambapo alishiriki shughuli mbali mbali za kujenga na kuimarisha chama pamoja na kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM 2010.
 Msafara wa Katibu Mkuu ukielekea Mtwara mjini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Mikindani mara baada ya kukabidhi leseni kwa madereva 70 wa boda boda waliohitimu mafunzo chini ya udhamini wa Mbunge wa Mtwara mjini Hasnain Murji
 Wananchi wa Mikindani mkoani Mtwara wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikabidhi pikipiki kwa vikundi vya Bodaboda zilizotolewa na Mbunge wa Mtwara mjini Hasnain Murji
 Mbunge wa Mtwara mjini Hasnain Murji akihutubia wakazi wa Mikindani baada ya kuwakabidhi leseni madereva 70 wa boda boda na kuwakabidhi pikipiki tatu kama mtaji wa kuendeleza vikundi vyao.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ukarabati wa ofisi ya CCM kata ya Majengo iliyochomwa moto wakati wa vurugu za gesi.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ukarabati wa ofisi ya CCM kata ya Majengo iliyochomwa moto wakati wa vurugu za gesi
 Katibu Mkuu wa CCM akiwasalimia wakazi wa kata ya Majengo alipotembelea kujionea maendeleo ya ukarabati wa ofisi ya CCM .
 Wananchi wakishangilia msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana aliyewasili mkoani Mtwara ambaye anategemewa kufanya mkutano mkubwa wa hadhara siku ya Jumapili tarehe 30 Novemba 2014.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimtwisha maji mama mmoja mkazi wa mtaa wa Mwera kata ya Chikongola baada ya kuzindua mradi wa kisima cha maji kilichofadhiliwa na Mbunge wa Mtwara mjini Hasnain Murji
 Katibu Mkuu wa CCM akiangalia kazi za kikundi cha wakina Mama wa Matopeni ambao wapo zaidi ya 200 na wanajishughulisha na shughuli mbali mbali za ujasiriamali Mtwara mjini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka jiwe la msingi la mradi wa ufugaji kuku wa mayai wa kikundi cha akina mama cha Rahaleo.
 Katibu Mkuu wa CCM akiangalia kuku wa mayai wanaofugwa na kikundi cha akina mama wa Rahaleo.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kushona viatu pamoja na fundi viatu Abeid Yusufu Likanga (ambaye ni mlemavu wa miguu) wa kata ya Rahaleo mkoani Mtwara.
 Katibu Mkuu wa CCM ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na viongozi wa chama wakiangalia maendeleo ya uchimbwaji wa mfereji unaopeleka maji baharini katika kata ya Shangani.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikara utepe kuashiria uzinduzi wa tawi la CCM Chuo cha Utumishi wa Umma kwenye ofisi za CCM wilaya ya Mtwara mjini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wanafunzi wa Chuo Cha Utumishi Mtwara mara baada ya kuzindua tawi lao la CCM.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikabidhi Katiba ya CCM kwa Katibu wa Tawi la Chuo Cha Utumishi Mwamvua Patrick.
 Katibu Mkuu wa CCM ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wajumbe wa wa halmashauri kuu ya wilaya ya Mtwara mjini kwenye kikao kilichofanyika ukumbi wa VETA
Katibu Mkuu wa CCM ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wajumbe wa wa halmashauri kuu ya wilaya ya Mtwara mjini kwenye kikao kilichofanyika ukumbi wa VETA ambapo alisisitiza wajumbe wasahau yaliyopita na kusimama kukijenga chama.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages