LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 19, 2014

KINANA AWATAKA WATU KUFANYA KAZI KWA BIDII

 
 Sista Maria Mfariji Milanzi wa Msista wa Benedikti wa Bikira Maria Msaada wa Kristo Ndanda Narunyu Novisiati akisoma taarifa ya mradi wa shamaba la mifugo Narunyu kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ambapo alielezwa kuwa shamba hilo lilianza na Ng'ombe 50 na sasa wana Ng'ombe 450,shamaba hilo linasaidia kupatikana kwa maziwa ,nyama na umeme unaotokana na kinyesi cha wanyama yaani Biogas.
Shamba hilo lililopo katika kijiji cha Kiwalala ,kata ya Kiwalala ,wilaya ya Lindi Vijijini

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kukamua  maziwa katika shamba la mifugo Narunyu katika kijiji cha Kiwalala jimbo la Mtama.
 Mbunge wa Jimbo la Mtama na ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa ya CCM na Waziri wa Mambo ya Nje Mheshimiwa bernard Membe akizungumza na wakati wa Mkutano Mkuu wa Jimbo ulioanyika Kiwalala
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungmza kwenye Mkutano Mkuu wa Jimbo la Mtama.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kubangua korosho kwenye mradi wa kikundi cha Wanawake  cha kubangua Korosho Nyengedi.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kitabu cha utekelezaji wa ilani ya CCM Jimbo la Mtama wakati alipopita kuwasalimia wananchi.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja  na Mh.Bernard Membe Mbunge wa Jimbo la Mtama na ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM na Waziri wa Mambo ya nje wakiwa kwenye picha ya pamoja na Makatibu wa Matawi wakati wa zoezi la kukabidhi baiskeli.
 
 Mbunge wa Jimbo la Mtama na ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM na Waziri wa Mambo ya nje Ndugu Bernard Membe akizungumza na wananchi wa kijiji cha Nyangamara.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Nyangamara
 Zahanati ya kijiji cha Litipu kata ya Nyangamara ikiwa katika hatua nzuri za ujenzi ambapo inategemewa kukamilika hivi karibuni.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kuchimba mtaro utakaolazwa bomba la maji katika mradi wa maji wa Nyangamara mjini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kujenga tenki la maji pamoja na Mbunge wa Jimbo la Mtama na ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa ya CCM na Waziri wa Mambo ya Nje Mh. Bernard Membe katika kijiji cha Nyangamara.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akicheza ngoma pamoja na Mbunge wa Mchinga Ndugu Said Mtanda wakati wa kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye uwanja wa mikutano Chiuta.
 Sehemu ya wakazi wa Chiuta wakiwa wamejazana kwenye mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa Chama Ndugu Abdulrahman Kinana
 Mbunge wa Jimbo la Mtama na ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa ya CCM na Waziri wa Mambo ya Nje Mh. Bernard Membe akiwapa salamu wakazi wa Chiuta ambapo aliwaambia kwamba upinzani hautochukua jimbo lolote mkoani Lindi.
Mbunge wa Jimbo la Mchinga Ndugu Said Mtanda akiwahutubia wakazi wa Chiuta kwenye mkutano mkubwa wa hadhara ambao Ndugu Abdulrahman Kinana alikuwa mgeni wa heshima.
 Wananchi wakisikiliza mkutano.
 Kaatibu wa NEC Itiakdi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Chiuta ambapo aliwaambia Chiuta ni nyumbani na aliwataka watu wachukue tahadhari na vyama visivyo na sera wala dira.
 Mwenyekiti wa CCM Mzee Ally Mtopa  akitoa salaam chache kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kuhutubia wakazi wa Chiuta.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wakazi wa Chuta ambapo aliwaambia kuwa maendeleo yanakuja kwa kufanya kazi na kujituma, ambapo aliwaambia kila nchi itaendelezwa na watu wake.
 Sehemu ya watu wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.

 Kila mtu alitaka kusikiliza na kuona.
 Mbunge wa Jimbo la Mtama na ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM na Waziri wa Mambo ya Nje Mh. Bernard Membe akizungumza na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Chiuta.
 Watu walikuwa makini sana kusikiliza mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akimkabidhi baiskeli katibu wa Tawi la Nambau LIndi Vijijini.

 Wanachama wapya wakila kiapo
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisoma kiapo kwa wanachama wapya waliojiunga na CCM katika kijiji cha Chiuta.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akitoa maelezo ya namna CCM ilivyojipanga kutatua kero za wananchi Chiuta ambapo kero zao kubwa ni kutaka Mawaasiliano ya Simu,  na kituo cha afya.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages