LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 19, 2014

DK. SLAA KWISHA KAZI, SASA AWA KIPOFU KAONA MWEZI KUHUSU ZIARA YA RAIS KIKWETE CHINA

Siku zote tunajua kuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Bwana Wilbroad Slaa ni mtu mwongo, mnafiki na mzandiki ambaye moja ya sifa zake ni kupora na kuoa mke wa mtu.

Lakini sasa amekuwa kipofu aliyeona mwezi. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Alhamisi, alidai kuwa amefanikiwa kunasa ratiba ya Mhe. Rais Jakaya Kikwete kwenye safari yake ya China na kubwata mambo mengi kuhusu ratiba hiyo.

Tatizo langu mimi ni uongo wa Bwana Slaa kuwa ametumia mbinu zake kunasa ratiba hiyo. Kwa nini nasema kuwa kauli hiyo ya Slaa ni uongo na kuwarubuni wananchi.

Ukweli ni kwamba ratiba ya Mhe. Rais mahali popote siyo siri. Ni jambo la wazi kabisa ambalo linaafikiwa baada ya watu wengi kushirikisha katika maandalizi ya ratiba hiyo.

Hivi tunavyozungumza ratiba ya Mhe. Rais kwa ajili ya safari ya China imechapishwa tayari kwenye kitabu. Na siyo ratiba tu, delegation nzima ya nani Mhe. Rais anaambatana nao inajulikana, tena kwa majina na nafasi zao, kwa sababu hili siyo jambo la siri.

Sasa Slaa anavyowaeleza watu kuwa amefaniki kunasa undani wa ratiba ya Rais Kikwete kule China anajaribu kumdanganya nani? Huyu ni mtu ambaye anajaribu kuwa kiongozi wa Watanzania na bado hana aibu wala aya kuwadanganya Watanznia hao hao kwa jambo lililo wazi. 

Tabia hiyo inathibitisha dharau ya Bwana Slaa kwa sisi Watanzani. Ni mtu ambaye hafai kuwa kiongozi, kwa sababu kiongozi hawezi kuwa mtu mwongo na mzandiki.

 Na tumesikitishwa sana na waandishi wa habari, kwani wamekubali kulishwa kila kitu na tena bila kufikiria na kuuliza maswali wanaripoti katika vyombo vyao na kushiriki kuudanganya umma wa watanzania.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages