LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 17, 2014

CCM YAUNGA MKONO KWA ASILIMIA MIA MOJA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA.

HALMASHAURI Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC) imemaliza kikao chake cha siku mbili chini ya Mwenyekiti wa CCM Dkt. JAKAYA KIKWETE ambapo pamoja na mambo mengine imepokea taarifa ya mchakato wa Katiba na kulipongeza bunge hilo.
Aidha imeunga mkono kwa asilimia mia moja Katiba hiyo pendekezi na kuwataka wananchi waisome,kuitafakari na wakati ukifika wajitokeze kwa wingi na kupigia  kura ya ndio.
Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Dodoma, Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi ndugu NAPE NNAUYE amesema   NEC wamelipongeza Bunge hilo  kwa kazi nzuri iliyofanya.


No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages