LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 21, 2014

KINANA ARINDIMA KIBAHA VIJIJINI, MAELFU YA WANANCHI WAHUDHURIA MKUTANO WAKE MLANDIZI

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimia wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Mtongani kata ya Kilangalanga ambapo alitoa maoni yake kuhusu Muungano.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa Mlandizi, Jimbo la Kibaha kijijini ambapo aliwasisitiza wananchi hao kuiamini CCM kwa maendeleo yao na pia kupeleka watoto shule za sekondari na kujiandikisha kwenye mfuko wa afya ya jamii.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia mamia ya wakazi wa Mlandizi kwenye viwanja vya shule ya msingi Mtongani kata ya Kilangalanga ambapo aliwaambia wasibabaike na wapinzani kwani hawapo kwa ajili ya maslahi ya watu na maendeleo yao.
 Mbunge wa Jimbo la Kibaha vijijini Ndugu Hamoud A. Jumaa akielezea maendeleo yaliyofanyika katika miradi mbali mbali jimboni kwake.
 Katibu wa CCM mkoa wa Pwani Joyce Masunga akiwasalimia wakazi wa Mlandizi wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Mtongani.
 Diwani wa Kata ya Kilangalanga  Fatma Shari maarufu kama Mama Kisebengo akihutubia wananchi wa kata yake wakati wa Mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na mamia ya watu .
 Mradi wa maji wa Boko Mnemela unaogharimu zaidi ya shilingi milioni 490 uawasaidia zaidi ya wakazi 4500.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiranda mbao baada ya kufungua shina la wakereketwa  la mafundi seremala  Tawi la Mshikamano.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimbeba mtoto Ashraf Wazir wa Mlandizi.
 Wananchi wa Shina la Wakereketwa mafundi Seremala wakiwa wamejipanga wakati wa zoezi la ufunguzi wa shina lao leo Mlandizi.

Mganga Mkuu wa Wilaya Dk. Victorina Ludovick (kulia)  akimuongoza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kushoto) kwenda kwenye kituo cha afya cha Mlandizi ambap pamoja na kushiriki ujenzi wa chumba cha kuhifadhia maiti, Katibu Mkuu alishiriki kupanda miti na kupokea taarifa kutoka kwa Mganga Mkuu .


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakishiriki ujenzi wa chumba cha kuhifadhia maiti katika kituo cha Afya cha Mlandizi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza wakati wa ufunguzi wa Ofisi ya Baraza la Ardhi usuluhishi kata ya Mlandizi. (Picha zote na Adam Mzee)

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages