LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 25, 2014

CRAWFORD SMITH FOUNDATION YAKUSUDIA KUSAMBAZA HUDUMA YA MAKTABA KWA WENGI

 Kutoka kushoto ni  Bw. Steven Smith,  Bi Ann Hanin, Mhe.  Balozi   Tuvako Manongi na Bibi Judith Smith


NA MWADISHI WETU, NEWYORK
Baada ya  kuridhishwa  na matumizi mazuri  na mafanikio makubwa ya    Maktaba yao ya kwanza waliyoifungua mwaka 2009 katika  kijiji cha Ngongongare   Mkoani Arusha.


Taasisis isiyo ya kiserikali ya  The Crawford Smith Foundation yenye   makazi yake  nchini Marekani na  ambayo ndiyo inayosimamia mradi wa  uanzishwa na uendeshaji wa Maktaba hususani katika maeneo ya   vijijini,   sasa inakusudia kujenga maktaba  nyingine sita katika maeneo mbalimbali  nchini Tanzania.

 Maktaba  hiyo ya kwanza na ya aina yake  na ambayo imepewa jina la  Jifundishe Free Library,   si tu inatoa huduma za vitabu vya kiada na ziada  kwa watumiaji  ambao ni kuanzia wale wa shule za awali, msingi, sekondari na hata vyuo vikuu, bali pia imekuwa kituo   ambacho  kinawasaidia wanawake na vijana   kujifunza  stadi mbalimbali zikiwamo za ujasiliamali,  vyama ya  kuweka na kukopa, huduma za  kinga ya afya, huduma za   internet na  mafunzo  ya ziada ambayo yamekuwa yakitolewa na wataalamu wa kujitolea kutoka nje na ndani ya  Tanzania.

Hayo yameelewa na Viongozi wakuu wa Taasisi hiyo ya  The Crasford Smith Foundation wakati  walipofika na kufanya Mazungumzo  na   Balozi Tuvako Manongi Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.

 Kwa mujibu wa  maelezo ya Bw. Steven Smith aliyekuwa amefuatana na Mke wake  Bibi. Judithi Smith   amesema kuwa  mwitikio mkubwa  na matumizi sahihi na endelevu vya  Jifundishe  Free Library  na matokeo mazuri ya wanafunzi katika mitihani  yao,  kumewafanya  watambue ni kwa kiasi gani huduma hiyo  muhimu  inahitaji  kusambazwa  katika maeneo mengine hasa ya vijijini. Lengo  likiwa ni kuwafikia na kuwapatia huduma hiyo  wasio kuwa na uwezo wa kuipata kwa urahisi.

Mradi huo wa  Maktaba  licha ya kutoa huduma mbalimbali,  lakini umekwenda mbali zaidi kwa kutoa ufadhili  wa masomo  ya Chuo Kikuu kwa wanafunzi  wanne hadi sasa. baadhi ya wanafunzi hao wamerudi na kutoa mchango wao  katika   Maktaba hiyo na jumuiya inayoizunguka.

Baadhi ya  maeneo ambako wanakusudia kupelea huduma hiyo muhimu ya maktaba ni  Kisarawe , Chunya , Iringa,  Morogoro na  Kilimanjaro.  Aidha wakuu hao wameeleza  kuridhidhwa kwao na  Ushirikiano wanaoupata kutoka kwa viongozi mbalimbali wa Serikali  akiwamo  Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete,  baadhi ya   Makampuni ambayo yameonyesha nia ya kushirikia na Taasisi hiyo katika  utoaji wa huduma hiyo, na vilevile mwamko na moyo  wakujitolea wa watanzania  katika maeneo wanayokusudia kuanzisha maktaba  hizo.


Kwa upande wake,  Mhe. Balozi   Balozi Manongi aliishukuru Taasisi hiyo kwa mchango wake mkubwa na ambao umeonyesha  mafanikio na mabadiliko makubwa kwa jamii inayohudumiwa. Akasema Tanzania inatambua umuhimu wa maktaba katika mustakabali mzima wa elimu na mafunzo na kwamba mchango wa taasisi zisizo za kiserikali unakaribishwa sana.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages