LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Apr 22, 2014

MAKAMU WA RAIS DK. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA 28 NIMR NA KONGAMANO LA WANASAYANSI WATAFITI LEO



 Makamu  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akizindua rasmi mkutano Mkuu wa mwaka wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Tanzania (NIMR) na kongamano na Wanasayansi wataifi. Kongamano hilo lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam, limeandaliwa na Taasisi hiyo ya (NIMR).
 Mkurugenzi wa NIMR, Dk. Mwele Malecela akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.
 Sehemu ya Wanasayansi Watafiti wakifuatilia utafiti huo.
 Mkurugenzi wa NIMR, Dk. Mwele Malecela akimsaidia Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilali kufungua moja ya mikakati aliyoizindua.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionesha vitabu alivyozinfua vya Mpango wa Mkakati wa Nne wa Utafiti Bora wa Afya,
Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilali akimkabidhi tuzo ya Mwanasayansi Bora wa mwaka kitaifa wa masuala ya afya, kwa Dk. Steven Magesa (kulia) wakati wa mkutano Mkuu wa mwaka wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Tanzania (NIMR) na kongamano na Wanasayansi wataifi ulioanza jana Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa Baraza la NIMR, Samwel Masele.
Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilali akimkabidhi Tuzo ya Mvumbuzi Bora wa Mwaka Kitaifa, Dk. William Kisinza (kulia) wakati wa mkutano Mkuu wa mwaka wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Tanzania (NIMR) na kongamano na Wanasayansi wataifi ulioanza jana Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa Baraza la NIMR, Samwel Masele.
 Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilali akimkabidhi tuzo ya Mwanasayansi Bora wa mwaka wa Afrika wa masuala ya afya, kwa Prof. Wenceslaus Kilama (kulia) wakati wa mkutano Mkuu wa mwaka wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Tanzania (NIMR) na kongamano na Wanasayansi wataifi ulioanza jana Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa Baraza la NIMR, Samwel Masele.

 Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilali (wapili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Washindi wa tuzo za Mwanasayansi Bora wa mwaka kitaifa wa masuala ya afya, kwa Dk. Steven Magesa (kushoto) Mwanasayansi Bora wa mwaka wa Afrika wa masuala ya afya, Prof. Wenceslaus Kilama (wapili kushoto) na Tuzo ya Mvumbuzi Bora wa Mwaka Kitaifa, Dk. William Kisinza (kulia) wakati wa mkutano Mkuu wa mwaka wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Tanzania (NIMR) na kongamano na Wanasayansi wataifi ulioanza leo Dar es Salaam.
Baadhi ya Wafanyakazi wa NIMR katika picha ya pamoja na mgeni rasmi

 Picha na viongozi mbalimbali.
Meza kuu ikiwa katika picha ya Pamoja na Makamu wa Rais, Kutoka kulia ni Ni Mkurugenzi wa NIMR, Dk. Mwele Malecela, Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilali, Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kebwe Steven Kebwe na Mwenyekiti wa Baraza la NIMR, Samwel Masele.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages