LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Dec 3, 2013

KINANA AWASILI MBEYA VIJIJINI MCHANA HUU

 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi zahanati ya Shamwengo,Kata ya Inyala, Mbeya Vijijinikiwa ni shughuli yake ya kwanza kufanya baada ya kuanza ziara yake mchana huu katika wilaya ya Mbeya Vijijini. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya hiyo Dk. Norman Sigala
 Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose  Migiro akishiriki ujenzi  zahanati ya Shamwengo Kata ya Inyala,Mbeya Vijijini
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akikagua ujenzi wa  mradi wa maji Kata ya Iwindi Mbeya Vijijini
 Kinana (aliyeshika tangi kushoto) akichungulia kina cha tanki, wakati akikagua ujenzi wa mradi wa maji kata ya Iwindi, Mbeya Vijijini
 Kinana akikatiza mitaa wakati akienda kwa mjumbe wa shina namba moja, Mtaa wa Nsalala, Barabara ya Tunduma. KUshoto ni Mkuu wa wilaya ya Mbeya Vijijini Dk. Norman Sigala
 Mjunmbe wa Shina namba moja, Lidya Mwangoka akifungua kikao cha shina lake, kilichohudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (watatu kusho), Kushoto ni Dk. Asha-Rose
Kinana akila mhindi nyumbani kwa balozi wa shina namba moja, Lidya Mwangoka, Mbeya Vijijini. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM Mbeya (V) Ipyana Seme
 Kinana akizindua shina la wakereketwa vijana wa CCM, Mshikamano Nsalala, Mbalizi, Mbeya Vijijini
 Wananchi mjini Mbarali Mbeya Vijijini wakiwa wamejipanga barabarani kushuhudia msafara wa Kinana
 Kinana akiongoza msafara wake katika barabara ya Mbalizi, Mbeya kwenda ukumbini kuendesha kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM wiyala ya Mbeya Vijijini. Baadhi ya viongozi alio nao ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk Asha-Rose Migiro na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye
Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Mbeya Vijijini wakiwa ukumbini mjini Mbalizi tayari kuzungumza na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages